Monday 27 July 2015

KAJALA,WOLPER NA IRENE UWOYA WAKUTANA KWENYE FILAMU YA WAKE UP

 Kwa mara ya kwanza tangu Tanzania imeanza,muandaaji wa filamu Manaiki Sanga anawakutanisha mastaa wa filamu na muziki zaidi ya 30 na kucheza filamu kubwa Africa Mashariki "WAKE UP"
 Filamu hiyo ambayo imeandikwa na kuongozwa na muandishi mwenye jina kubwa bongo Leah Mwenda Mseke ni miongoni mwa filamu bora zitakazowaacha watu vinywa wazi kwa namna ilivyochezwa kwa kiwango cha juu sanaaa
 Amesema ikitoka watu wanunue waone jinsi ili mastaa hao walivyocheza kwa kiwango kikubwa watoto wa mjini wanasema wakiwa kwenye ubora wao
 Filamu hiyo inatoka mwisho wa mwezi huu na itafanyiwa uzinduzi wa kihistoria hivyo mashabiki mnaombwa mkae tayari



Saturday 4 July 2015

MLELA:MAMA NA MWANA NI FUNZO KWA JAMII INYOWATENGA WATOTO WENYE UTINDIO WA UBONGO

 Zikiwa zimebaki siku chache filamu mpya ya mcheza filamu Yusuph Mlela inayokwenda kwa jina la Mama na Mwana kuingia sokoni,Mlela amesema filamu hiyo ni funzo kwa jamii ya kitanzania inayowatenga watoto wenye utindio wa ubongo.
Mlela amesema filamu hiyo inatoa picha halisi ya mateso na maumivu yanayompata mama anaezaa mtoto mwenye utindio wa ubongo

"filamu ya mama na mwana inahusu mama aliezaa mtoto mwenye utindioa wa ubongo anavyopata shida kwenye ndoa yake baada mume kumguka na kumpa maneno makali<
kwenye filamu hiyo ambayo inasambazwa na steps entertainment Mlela amewashirikisha wasanii wengi akiwemo Wastara na Hemed,sio ya kukosa ikitoka