Zikiwa zimebaki siku chache filamu mpya ya mcheza filamu Yusuph Mlela inayokwenda kwa jina la Mama na Mwana kuingia sokoni,Mlela amesema filamu hiyo ni funzo kwa jamii ya kitanzania inayowatenga watoto wenye utindio wa ubongo.
Mlela amesema filamu hiyo inatoa picha halisi ya mateso na maumivu yanayompata mama anaezaa mtoto mwenye utindio wa ubongo
"filamu ya mama na mwana inahusu mama aliezaa mtoto mwenye utindioa wa ubongo anavyopata shida kwenye ndoa yake baada mume kumguka na kumpa maneno makali<
kwenye filamu hiyo ambayo inasambazwa na steps entertainment Mlela amewashirikisha wasanii wengi akiwemo Wastara na Hemed,sio ya kukosa ikitoka
No comments:
Post a Comment