Wednesday 15 March 2017

LUTWAZA KUZIBA PENGO LA KANUMBA KWENYE FILAMU


Mcheza filamu anaefanya vizuri kwenye tasnia Philemon Lutwaza ametajwa kuwa ndio mwenye jukumu la kuziba pengo la marehemu Steven Kanumba kutokana na kufanana kwa muonekano na uigizaji wake

Wakifunguka kiafrika bila hofu yoyote baadhi ya mashabiki wamesema Lutwaza anaweza kuziba pengo kwani anajituma sana kwenye kazi na hajatofautiana sana na marehemu Kanumba

"Unajua huyu Lutwaza anacheza vizuri sana na nina vutiwa na uigizaji wake anajua yani nikimuangalia namuona Kanumba kabisa"
Lutwaza anaonekana kwenye filamu ya Yai viza ambayo imeandaliwa na muongozaji wa filamu nchini Sulesh Mala

No comments:

Post a Comment