Saturday 6 December 2014

WATANZANIA WALILIA ADAMU KUAMBIANA KWENYE FILAMU YA LIKWATA

 Filamu ya Likwata iliyoingia mtaani ijumaa hii imewapa wakati mgumu mashabiki wa filamu Tanzania baada ya kuona jinsi marehemu Adamu kuambiana alivyoitendea haki filamu hiyo na wengine wamefika mbali na kusema mungu amemchukua mapema sana msanii huyo aliekuwa kivutiao kwa wengi kutokana na busara zake.
Kwenye filamu hiyo yumo pia mcheza filamu mwenye jina kubwa uswahilini wakiamini kuwa ndio anaongoza kwa kuchamba kwenye filamu Riyama Ally uku pembeni akiwepo kaka mtanashati Niva na wasnii wengine wengi

Kama kweli we ni mpenzi wa filamu za kitanzania nunu nakala halisi uone jinsi marehemu Adamu Kuambiana alivyowaliza watu kwenye filamu hii ambayo ni moja kati ya filamu za mwisho kabisa kwa mkongwe huyo kucheza

No comments:

Post a Comment