Wednesday 31 December 2014

MASTAA SABA WAKIKE WALIOFANYA VIZURI KWENYE FILAMU KWA MWAKA HUU 2014

WASTARA JUMA
 Namba moja inakwenda kwa Wastara Juma,kwa mwaka huu amecheza filmau sita mbili zikiwa za kwake filamu hizo ni Gumzo,Dr Max,Last Decision,Uaminifu Dhaifu,Njia Panda na Mama kijacho ,pia amepata tuzo kama msanii bora wa kike kwa mwaka huu kupitia tuzo za action and cut na tuzo ya heshima aliyopewa na team wastara,pia amefanikiwa kucheza filamu nchini London chini ya kampuni ya didas entertainment

SALMA JABU NISHA
 Namba mbili inakwenda kwa Salma Jabu Nisha ambae kwa mwaka huu ameweza kufanya filamu zake tatu na zote zimefanya vizuri na kumuongezea mashabiki zaidi,filamu hizo ni Gumzo,Zena na Betina pamoja na Hakuna Matata aliyofunga nayo mwaka,pia amepata tuzo ya mchekeshaji bora kwenye tuzo za action and cut kwa mwaka huu


SHAMSA FORD
 Namba tatu inakwenda kwa Shamsha Ford kwa mwaka huu ameweza kujizolea umaharufu mkubwa kupitia filamu ya Chausiku na kufanya filamu hiyo kuvunja rekodi ya mauzo ambayo aliwai kuifikia marehemu Kanumba,pia ameshiriki filamu ya Hukumu ya ndoa Yangu


RIYAMA ALLY
Namba nne inakwenda kwa Riyama Ally,kwa mwaka huu amecheza filamu nyingi sana na amejizolea umahaarufu mkubwa kwa mashabiki,filamu kama kigodoro kantangaze,Msuto Daily,Likwata,pamoja na Najua kua zimemuweka nafasi ya juu sana,pia ameweza kushiriki filamu ya kimataifa ya Mateso yangu Ughaibuni ambayo imefanyika nchini London


ODAMA
Namba tano imeshikiliwa na mwana mama Odama kwa mwaka huu amecheza filamu kama Jicho langu na Inside ambazo zote zimefanya vizuri sokoni,pia kwa mwaka huu hakupata skendo yoyote mbaya


ESHA BUHETI
Namba sita inakwenda kwa Esha buheti ambapo kwa mwaka huu amefanya vizuri kwenye filamu kama taliq swalaa na tugawane maumivu pia amechukua tuzo mbili za filamu


WELU SENGO
Welu Sengo amefanya vizuri kwa mwaka huu kupitia filamu ya Hukumu ya Ndoa yangu pia amepata tuzo ya action and cut kama msanii anaesapoti muhusika mkuu kwenye filamu kupitia filamu ya Matrida

1 comment: