Tuesday 30 December 2014

BONDI, WASTARA PENZI LAO KIZUNGU MKUTI


Akizungumza na Uwazi, mpenzi wa Wastara anayetambulika kwa jina la Bondi Bin Salim alidai kuwa yupo kwenye mchakato wa mwisho wa kutoa mahari kwa ndugu wa msanii huyo kiasi cha shilingi milioni 5 pamoja na pete za dhahabu ili aweze kuwa na Wastara.
Alisema kuwa maamuzi ya kutoa posa yamekuja baada ya kuona kila mmoja anaweza kuishi na mwingine kwani wameshasomana kwa muda mrefu.
“Najua si jambo la watu kuhoji sana kwa sababu ndoa ipo na kila mtu atafanya hivyo, nina hela ya mahari tayari na siku ikipangwa ya kutoa tutafanya hivyo lakini ninachowaza sasa ni kuona nafanya vipi ili harusi yangu iwe ya kipekee na zoezi hili tutalifanya mwakani,”
Bond na Wastara wamecheza filamu ya uaminifu dhaifu ambayo inasambazwa na kampuni ya steps intertainment jipatie nakala yako sasa uone walichokifanya

No comments:

Post a Comment