Saturday 13 December 2014

SOMA ALICHOKISEMA Timoth Conrad Kachumia BAADA YA KUPATA TUZO UKO U.S.A

Nina masikitiko kidogo, nilitegemea wanasanaa wenzangu wangenipa sapoti kwa mafanikio haya ya kuipeperusha bendera ya nchi yetu nchini marekani, lakini imekuwa tofauti.
Ila Mama na Baba yangu walinambia "MWIKO KUKATA TAMAA" nitaipigania nchi yangu mpaka kieleweke, nafurahi marafiki zangu wa facebook, instagram, twitter mnanipa sapoti na kunitia moyo lakini huko mtaani kwa baadhi ya wenzangu du utasikia "aah anajifanya mjuaaaji eti limuvi lake limeshinda tuzo marekani basi ndio linajidaaai"
Anyway tungoje Diamond Apate tuzo nyingine ndio tukampokee tena airpot kwa shangwe na vigere gere.
Kwa wale watu wangu wanguvu napenda niwape taarifa kuwa ndugu yenu naingia tarehe 16 siku ya jumanne saa saba kamili mchana. Mkipata nafasi msisite kuja kunipokea na LITUZO LANGU MKONONI.
Asante sana.
We Make We Believe.

No comments:

Post a Comment