Monday 10 November 2014

ESHE AWANANGA MASTAA BONGO MOVIE

Staa wa filamu za Kibongo,  Eshe Buheti ameibuka na kuwananga mastaa wa kike waliobaki kwenye Kundi la Bongo Movie Unity kuwa hawajielewi na kazi yao ni majungu tu 

Eshe amesema  kuwa imefikia hatua baadhi ya wasanii hao hawasalimiani wanapokutana misibani kisa ni yeye kujitoa kwenye kundi, kituambacho haoni kama kina tija.

“Nawashangaa wasichana wenzangu naona hawajielewi tu ni kama vipofu kwani kwa ilipofikia mwisho tutapigana kwa sababu hata tukikutana misibani wananuna hiki ni kichekesho, mbona wakina Monalisa hawana kundi akina Riyama na wanafanya kazi kama kawaida? Badilikeni”, alisema Eshe pasipo kuwataja majina akidai wanajijua.

No comments:

Post a Comment