Thursday 29 January 2015

Wastara Awa Balozi Wa Medo Katika Kuchangia Elimu


 Mwigizawa filamu Bongo, Wastara Juma,  jana amepata heshima baada ya kupata nafasi ya  kuwa balozi wa Morogoro Education Devolopment Organization (MEDO) kwa ajili ya kuchangia elimu kwa watoto wa kike.
Hafla hiyo fupi ilifanyika  katika ukumbi wa Hotel ya Tamal, jijini Dar, ambapo Wastara alisaini mkataba wa kazi hiyo rasmi inayohusu uchangishaji wa fedha kwa jukumu hilo ambapo kaulimbiu yake ni  ‘500/= Yatosha Kunipa Elimu’.  Namba ya  uchangiaji katika mfuko huo kwa wenye nia ya kufanikisha mradi huo ni 0713  834540, 0787 747327 na 0769 224726.
PICHA: Meneja wa mradi huo, Bertha Gama (kushoto) na mwenyekiti wake Silas Masui (katikati) wakiwa na Wastara Juma.
Hili ni jambo jema na la mfano, tuwaunge mkono.

No comments:

Post a Comment