Friday 24 October 2014

CATHY, KUBADILI JINA KISA LINA MKOSI

MKONGWE wa filamu kitambo, Sabrina Rupia ‘Cathy’ amesema kuwa jina analotumia katika sanaa lina mkosi hivyo yuko kwenye mkakati wa kulibadilisha na kujipa jina lingine labda linaweza kumkaa vizuri.


Cathy amesema anaona jina hilo lina mkosi kwa sababu linazungumzwa vibaya na baadhi ya wasanii wenzake hata kama kuna kitu ambacho hakijui ni lazima lihusishwe jina lake kitu ambacho anakiona kama jina hilo lina nuksi.
“Unajua naona jina hili lina mkosi kwa sababu kitu kifanyika labda mimi nimepita tu basi litatajwa jina langu kitu ambacho mimi sikipendi na kuona labda lina matatizo jamani, haliko sawa kuendelea kuwa nalo,” alisema Cathy huku akidai yuko katika mikakati ya kutafuta jina lingine zuri ambalo anaona linamfaa.

Staa huyo mkongwe ameonesha uwezo mkubwa kwenye filamu kama Big Daddy ya marehemu kanumba na Chausiku ya JB inayofanya vizuri sokoni ikisambazwa na kampuni kubwa ya filamu nchini stepsentertainment

No comments:

Post a Comment