Baadhi ya wasanii wanaotajwa kuunda kundi hilo kwa mujibu wa chanzo chetu makini ni pamoja na Devotha Mbaga, Salama Salmin ‘Sandra’, Halima Yahya ‘Davina’ na wengineo.
“Yaani sasa hivi haya makundi mawili kuna
vita kali sana, kila moja linataka lionekane kwamba lina nguvu kuliko
lingine, hata jina la Bongo Movie Unity limebadilishwa sasa hivi
linaitwa Bongo Movie Stars
Mussa Issa ‘Cloud’ alikiri kubadilishwa jina kwa Bongo Movie Unity na
pia amesikia habari za kuwepo kwa kundi la Ukawa wakati Steve Nyerere
alisisitiza kuwa bado ni mwanachama wa Bongo Movie Unity na kwamba mtu
anayetaka kuwagombanisha wasanii anajulikana.
No comments:
Post a Comment